October 25, 2010

AHADI ZA WAGOMBEA UONGOZI WA NCHI, JE ZIPI ZINAZOTEKELEZEKA?


Ndugu zangu watanzania wakati zimebaki siku chache kupiga kura tumeyasikia mengi lakini leo tupime na kuangalia ni yapi yalioahidiwa na wagombea wa uraisi kutoka vyama mbalimbali vya siasa kama yatatekelezeka..... tumia haki yako ya msingi kumchagua kiongozi atakayekufaa..


AHADI ZA CHAMA CHA MAPINDUZI KUPITIA MGOMBEA WAKE MHESHIMIWA DR. JAKAYA KIKWETE



Kujenga reli mpya kutoka Dar es Salaam mpaka mikoa ya Kanda ya ziwa-Nzega, Tabora
  1. Mkoa wa Tanga kuwa Jiji la Viwanda- Tanga mjini
  2. Tabora kutumia maji ya Ziwa Victoria-Igunga
  3. Kulipa madeni ya chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (SHIRECU)- Shinyanga
  4. Kumaliza migogoro ya Ardhi nchini- Dodoma
  5. Wakulima kuacha kutumia jembe la mkono-Dodoma mjini
  6. Kuwapatia trekta wakulima -Kata ya Mrijo, Dodoma
  7. Wananchi kutoondolewa kwenye Ranchi ya Misenyi-Kagera
  8. Kujenga Uwanja wa Ndege Misenyi-Kagera
  9. Kupanua Uwanja wa Ndege Bukoba-Bukoba Mjini
  10. Kujenga uwanja wa ndege mkubwa Kigoma - Kigoma Mjini
  11. Mtukula kupatiwa umeme kutoka Uganda- Kagera
  12. Mikoa ya Kagera, Kigoma, Lindi, Rukwa na Ruvuma kuunganishwa katika gridi ya taifa ya umeme- Kagera
  13. Kuimarisha Takukuru kwa miaka mitatu-Kagera
  14. Hukumu kwa waliopatikana na hati ya kuua albino- Mbeya
  15. Kununua meli kubwa kuliko MV Bukoba-Kagera
  16. Kuanzisha benki ndogondogo kwa ajili ya wajasiriamali
  17. Serikali kuvisaidia vyama vya ushirika-Mwanza
  18. Kuimarisha usalama Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika kwa kupeleka kikosi maalum chenye vifaa kupambana na wahalifu-Mwanza
  19. Wilaya ya Geita kuwa hadhi ya mkoa Januari mwakani- Geita
  20. Kulinda muungano kwa nguvu zote-Pemba
  21. Kuwajengea nyumba waathirika wa mafuriko Kilosa-Morogoro
  22. Kununua meli mpya kubwa Ziwa Nyasa-Mbeya mjini
  23. Kujenga bandari Kasanga –Rukwa
  24. Kumaliza tatizo la walimu miaka mitano ijayo - Songea
  25. Kufufua mgodi wa makaa ya mawe Kiwira -Mbeya
  26. Kuzuia hatari ya kisiwa cha Pangani kuzama- Tanga
  27. Kununua bajaji 400 kwa ajili ya kubeba wajawazito hasa vijijini- Iringa
  28. Kujenga barabara yenye kiwango cha lami kutoka Same mpaka Kisiwani –Kihurio na kuiunganisha na barabara kuu ya Moshi -Dar es salaam- Same mkoani Kilimanjaro
  29. Kumaliza tatizo la maji katika wilaya ya Same-Same Mjini
  30. Kuboresha barabara za Igunga -Tabora
  31. Kusambaza walimu 16,000 katika shule za sekondari zenye upungufu makubwa wa walimu- Kisesa Magu
  32. Kununua vyandarua viwili kwa kila kaya- Mbeya Mjini
  33. Kuzipandisha hadhi hospitali maalumu saba nchini kuwa za rufaa ili kuipunguzia mzigo Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MHN)-Hydom Manyara
  34. Kulinda amani nchini kwa kuzuia chokochoko za kidini, kikabila na kisiasa- Musoma
  35. Kulinda haki za walemavu- Makete
  36. Kujenga baabara ya Njombe- Makete kwa kiwango cha lami,urefu wa kilomita 109- Iringa mjini
  37. Kujenga barabara Musoma–Mto wa Mbu Arusha-Arusha
  38. Kuanzisha jimbo la Ulyankulu- Shinyanga Mjini
  39. Kujenga barabara ya lami Manyoni-Kigoma– Kaliua,Tabora
  40. Kukarabati barabara ya Arusha Moshi-Arusha Mjini
  41. Kuboresha barabara ya Handeni, Kondoa,mpaka Singida-Dodoma
  42. Kuwafidia wanakijiji ng’ombe waliopotea wakati wa ukame mwaka 2009- Longido 45.Vijiji vyote vilivyoko kilomita 15 kutoka kwenye bomba kuu la mradi mkuu wa maji wa Ziwa Victoria-Shinyanga-Kahama kuunganishiwa maji - Shinyanga
  43. Tatizo la umeme kufikia kikomo Novemba mwaka huu mkoani Arusha –Arusha mjini
  44. Kukopesha wavuvi zana za kilimo-Busekera, Wilaya ya Musoma, .
  45. Kuwapatia maji wakazi wa Wilaya ya Longido- Longido
  46. Kujenga barabara ya lami kupitia pembezoni mwa Hifadhi ya Taifa ya Seregenti – Ngorongoro
  47. Utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya kilimo kuwasaidia wafugaji kuweza kupata na kutunza mifugo yao vizuri- Mbulu mkoani Manyara
  48. Kusambaza maji nchi nzima-Babati vijijini
  49. Kusambaza umeme, utoaji wa huduma za afya, na uboreshaji wa kilimo cha umwagiliaji na utoaji ruzuku kwa wakulima. mwaka 2010-2015-Babati vijijini Kuongeza mara tatu idadi ya wananchi wanaonufaika na ruzuku ya pembejeo za kilimo kwa mfumo wa vocha.-Iringa
  50. Kuhakikisha Isimani inapata maji ya uhakika- Iringa
  51. Kuiwekea lami barabara inayokwenda katika Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ambayo ndiyo hifadhi kubwa kuliko zote Tanzania-Iringa
  52. Kulinda usalama wa wananchi kwa ujumla ili kudumisha amani na sifa ya nchi-Ifunda
  53. kutokomeza malaria 2015-Bunda,mkoa wa Mara
  54. kuwapa wanawake nafasi zaidi-Kilolo ,Iringa
  55. ahadi kuisadia Zanzibar kuendeleza miradi mbalimbali ya kijamii-Kibandamaiti Mjini Zanzibar
  56. Kuipandisha hadhi hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar kuwa ya rufaa-Kabandamaiti mjini Zanzibar
  57. Kuisaidia Zanzibar kila panapohitajika msaada-Kibandamaiti
  58. Serikali kujenga upya bandari ya Mbambabay-Ruvuma
  59. Ununuzi wa Meli mpya yenye uwezo wa kubeba tani 400-Mbambabay Ruvuma
  60. kufufua chama kikuu cha ushirika cha wakulima wa Mbinga(MBICU) –Ruvuma
  61. Ahadi Rais wa Marekani Barack Obama kuimwagia misaada Tanzania –Ruvuma
  62. Ahadi hakutakuwa na umwagaji wa damu baada ya uchaguzi-Dar es Salaam
  63. Mtwara kuwa mji wa Viwanda –Mtwara
  64. Ahadi ujenzi wa kwanda cha dawa ya kuua viluilui vya mbu-Kibaha
  65. Hospitali ya Tumbi kuwa ya mkoa-Kibaha
Halmashauri ya manispaa ya Kibaha kutenga eneo maalumu la viwanda -Kibaha

NAYE MGOMBEA DR. WILBROAD SLAA KUPITIA CHADEMA


1.Kujenga nchi isiyo na ufisadi
2.Kufufua Tanganyika ili irejee mezani kujadili muungano na Zanzibar
3.Kufufua uchumi wa nchi kwa kutumia rasilimali zilizopo
4.Kukata asilimia 20 ya mshahara wa rais
5.Kupunguza mishahara ya wabunge kwa asilimia 15
6. Kuweka Mwenge wa Uhuru Jumba la Makumbusho
7. Kutoa huduma bora za afya bure
8. kufuta kodi ya vifaa vya ujenzi
9. Kuwalipa wazee wa EAC fedha zao ndani ya siku 100
10. Kubana matuzi Ikulu (Yuko tayari kula mihogo

PROF. IBRAHIMU LIPUMBA WA CUF

1.Elimu ya bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu
2.Kubana matumizi kwa kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri
3.Kuunda serikali shirikishi
4.Kusimamia rasilimali
5.Kuimarisha miundombinu
6. Kusimamia na kuboresha afya
7. Kuboresha kilimo, viwanda na uwekezaji
8. Kurudisha chakula cha bure mahospitalini

kwa vyama vingine vya upinzani sera zao zinafanana kwa asilimia  kubwa . tucheki na upande wa zanzibar kwa Chama Cha Mapinduzi (Dr.Shein)na chama cha CUF  Sharrif Hamad


kwa upande wa Dr Shein kaahidi mengi kama..

1) Kuboresha maisha ya wavuvi-Chakechake Pemba
2) Kusomesha wafanyakazi-Mnazi mmoja
3) Kipaumbele katika elimu -Unguja na Pemba
4) Kipaumbele katika afya-Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba.
5) Kuulinda Muungano- Wawi kisiwani Pemba
6)Kuleta mabadiliko Zanzibar-Pemba na Unguja
7)Kuboresha Bandari ya Zanzibar kwa kuijenga upya-Kibandamaiti
8)Kuboresha Maendeleo Zanzibar- Jimbo la Wete, Pemba
9.Ujenzi wa maktaba kubwa na nzuri Kisiwani Pemba- Mtambwe
10.Kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu Zanzibar- Kijiji cha Kambini Mchangamdogo
11.Kuimarisha miundombinu Kisiwa cha Pemba- Kijiji cha Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba
12.Kuhamasisha wawekezaji kuwekeza Pemba katika miradi mbalimbali-Makombeni Mkoa wa Kusini Pemba.
13.Ahadi eneo la Micheweni kuwa maeneo huru ya uchumi- Micheweni Kaskakzini Pemba
14. Kumaliza matatizo ya maji mkoani -Mkoani
15..Kujenga Bandari ya kisasa katika eneo la Mpiga Duri Unguja- Mkoani
16.Kuiamrisha makazi bora kwa Wazanzibar- Mkoani


na ndugu yetu wa CUF kaahidi haya..............

1. Zanzibar kuwa kama Hong Kong – Unguja
2.Kuendeleza mashamba ya Karume- Kibanda maiti
3. Kubadilisha katiba na kuunda katiba mpya ya muungano na Zanzibar- Pemba
4.Kubadilisha mfumo wa uteuzi makamishna wa tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC)- Unguja
5. Kuwaunganisha wazanzibari ili kujenga umoja, udugu na ushirikiano-Pemba
6. Kuwasilisha hoja ya kubadili katiba ya Zanzibar na ya Muungano-Viwanja vya Kibanda Maiti
7. Kuondoa bajeti ya ZEC isiwe chini ya waziri kiongozi na badala yake kuwa inajitegemea yenyewe- Pemba
8. Kuondoa ulazima wa mwenyekiti wa tume kuwa jaji na badala yake awe mtu anayejua sheria-Unguja
9. Serikali kuundwa na vyama vyote vilivyopata ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi- Unguja
10.Kujenga jamii yenye maelewano na umoja -Pemba
11.Kutokochagua kiongozi kwa urafiki bali kwa uwajibikaji na uadilifu -Unguja na pemba
12.Kudhibiti vyombo vya dola vinavyofanya kazi kwa matakwa ya watu binafsi -Kibanda maiti
13.Kukomesha rushwa-Mkanyageni Mkoa wa Kusini Pemba
14.Kuhakikisha ununuzi wa zabuni unakuwa wazi na wananchi kuruhusiwa kuhoji kuhusu zabuni-Jimbo la ole Pemba
15.Kuongeza kima cha chini cha mshahara hadi Sh150,000-Mkanyageni Pemba
16.Kubadili vikosi vyote vya usalama na kulipwa mishahara kima cha chini kulipwa Sh180,000-Chakechake Pemba
17.Kubadilisha kikosi cha KMKM kuwa kikosi cha mwambao-Wawi
18.Wazee kupanda daladala bure na wale wasiokuwa na watoto kulelewa bure-Majimbo ya Chakechake
19.Kufuta michango yote ya shule za msingi na sekondari, kila mwanafunzi kuwa na kompyuta na badala ya kuishia darasa la saba sasa kuishia kidato cha sita-Hoteli ya Bwawani
20.Kutoa kitambulisho cha kila Uzanzibari na kufuta cha Mzanzibari mkaazi- Uwanja wa Hospitali ya Mnazi Mmoja
21.Kila mzanzibar kupata pasi ya kusafiria- Hoteli ya bwawani Zanzibar
22.Kuanzisha shirika la ndege Zanzibar -Viwanja vya Kibanda maiti
23.Kupandisha uchumi wa Zanzibar kutoka 6.8 hadi 15 kila mwaka kwa Zanzibar -Unguja
24.Kutoa uhuru zaidi kwa vyombo vya habari pamoja na kusaidia uanzishwaji wa Baraza la Habari Zanzibar-Unguja na Pemba
25. Kuweka hadharani nambari yake ya simu - Viwanja vya Kibanda miti
26. Kubadili sheria ya uwekezwaji-Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar
27.Kila mwanafunzi kuwa na komputa yake-Viwanja vya Kibanda maiti
28.Akiwa rais hata waziri au mkewe atafungwa akiwa ametenda kosa-Viwanja vya Tibirizi Kisiwani Pemba
29.Kujenga bandari ya Mkokoto na Pemba ili kuweka usafiri wa haraka wa boti ziendazo kasi-Tibirizi Kisiwani Pemba
30. Ahadi kudhibiti kuvuja kwa mitihani- Unguja

October 23, 2010

MOSHI UNIVERSITY COLLEGE OF COPERATIVES AND BUSINESS STUDIES (MUCCOBS)





kwa wadau wote: Chuo cha Ushirika Moshi (MUCCOBS)  kimetoa fomu za kujiunga na mwaka wa masomo 2010/2011 download fomu hizo kwenye website yao; http://www.muccobs.ac.tz./

TWIGA STARS YAELEKEA SOUTH AFRICA

Twiga stars timu ya mpira wa miguu ya wanawake yaelekea South Africa. Timu hiyo itapita Botswana kwaajili ya kucheza mechi mbili kujipima nguvu. Watanzania wote tuwaunge mkono, tuwaombee dua warudi na ushindi wa kishindo. Tanzania nasi tunaweza!
 Twiga Stars itaikabili Banyana Banyana ya Afrika Kusini Oktoba 31, siku ambayo Watanzania watakuwa wakipiga kura kuchagua viongozi wao.

Twiga Stars watacheza mchezo huo wa ufunguzi wa michuano hiyo ya soka ya wanawake ya Afrika, wakiwa Kundi A ambalo linazo pia timu za Nigeria na Mali.

Kocha wa timu hiyo, Boniface Mkwasa alisema  jana kuwa watakosa haki yao ya msingi kama Watanzania ya kupiga kura, lakini watakuwa katika jukumu lingine la kuiwakilisha nchi yao katika fainali hizo, jambo  ambalo linawafariji.

Mchezo wa Twiga Stars na Banyana  utachezwa kwenye Uwanja wa Sinaba mjini Joharnesburg.

Akizungumza na Mwananchi  baada ya mazoezi yao  jana asubuhi ,  Mkwasa alisema wanasikitika kukosa haki yao ya msingi ya kuchagua viongozi wanaowataka kutokana na kuwa na jukumu hilo na hawawezi kuacha kushiriki fainali hizo kwani tayari ratiba imetolewa.

Alisema mbali ya kukosa nafasi hiyo kwa sasa wanaelekeza nguvu zao katika mchezo huo kwani macho na masikio ya Watanzania yatakuwa kwao, hivyo watahakikisha wanatumia vyema nafasi yao kwa nia ya kuilinda na kuipeperusha vyema bendera ya Tanzania.

"Ni kweli tunacheza siku ambayo taifa letu litakuwa katika shughuli ya upigaji kura na sisi kama Watanzania ambao tuna kila sababu ya kushiriki hatutaweza kufanya hivyo kutokana na kuwa na jukumu hilo,"alisema Mkwasa.

Alisema,"kikubwa kwa sasa wachezaji waelekeze nguvu zao katika fainali hizo wasiangalie masuala ya siasa kwani ratiba haiwezi kubadilishwa, hivyo sisi tutakuwa na jukumu lingine wakati wenzetu wakipiga kura."

Aidha Mkwasa alisema maandalizi kwa ajili ya safari yao yanakwenda vizuri na kwa sasa wameliachia shirikisho la soka nchini, TFF kuhusu safari yao na ameongeza kuwa endapo ratiba itakwenda kama ilivyopangwa watacheza michezo miwili ya kirafiki ya kimataifa kabla ya kuelekea Afrika Kusini.

Timu hiyo itaondoka nchini Jumapili ambapo kabla ya kuwasili Afrika Kusini itacheza na Zimbabwe pamoja na Swaziland michezo ya kirafiki ili kujiweka fiti zaidi.

Wakati huo huo, kocha wa timu ya wanawake ya Nigeria 'Super Falcon', Eucharia Uche anatarajia kutangaza kikosi cha wachezaji 21 kesho ambao wanatoka katika timu za U-17 na U-20 ambao watacheza dhidi ya Twiga Stars katika michuano hiyo.

"Nimeona wachezaji wazuri na wenye uwezo ambao wanatoka kwenye timu za vijana (U-20) na wataweza kutengeneza timu nzuri na ni matumaini yangu nilivyowaona katika mazoezi watasaidia kwa kiasi kikubwa katika uteuzi wangu wa mwisho na kila kitu kinakwenda vizuri kwa upande wa maandalizi na tuko tayari kwa fainali hizo,"alisema kocha huyo.


October 22, 2010

clocklink

www.clocklink.comweraaaaaaaaaaaaa!

KUWANIA UCHAGUZI MKUU OCTOBER31 MWAKA HUU

Watanzania wote tuungane katika kupiga kura ifikapo oktoba 31, tuchague kiongozi bora, mwadilifu, mzalendo tusiangalie sura , kabila, dini yake wala chama anachotoka kwa manufaa ya kuijenga Tanzania ya kesho, kura yako na yangu ndio itakayoamua kupata maisha bora au bora maisha


Rooney akalia kuti kavu Man United

<>
LONDON, Uingereza
MSHAMBULIAJI Wayne Rooney anakabiliwa na hatari ya kuondolewa kikosi cha kwanza cha Manchester United  baada ya kumkosoa kocha wake, Alex Ferguson.

Kutokana na kauli yake akipingana na Ferguson kwamba hakuwa majeruhi, sasa ni dhahiri Rooney anaweza kuachwa benchi kwenye mchezo wa leo dhidi ya West Brom.

Rooney, pia alimhoji kocha wake kwanini ameachwa benchi katika mechi mbili ilizocheza klabu hiyo.

Ferguson alisema  Rooney aliachwa benchi dhidi yaValencia na Sunderland kutokana na kuwa majeruhi wa kano ya goti, akidai kwamba mshambuliaji wake huyo aliwaficha madaktari wa klabu kuhusu ukubwa wa maumivu yake

Lakini, baada ya mechi ambayo England ilitoka suluhu 0-0 dhidi ya Montenegro  Jumanne,  Rooney alikana madai ya kocha wake.

Madai yake yaliungwa mkono na daktari wa timu ya taifa, Gary Lewin, ambaye alieleza:
"Ninachoweza kuzungumzia ni siku saba ambazo Wayne alikuwa kikosi cha England, alifanya mazoezi kila siku  na alikuwa fiti kwa mchezo.

"Ni kweli kwamba hajaichezea Man  United  kwa wiki mbili kabla ya mechi ya England na kilichotokea kwenye klabu yake (United ) ni  kati yake na kocha wake . Lakini, alipowasili hapa, alikuwa fiti na tayari kufanya mazoezi na kucheza."

Ferguson huenda alikuwa akimpumzisha na kumwepusha na kufuatiliwa mno na vyombo vya habari  na maisha yake binafsi, lakini sina shaka Rooney  alitaka kucheza."

Kocha huyo alikuwa na imani kuwa baada ya kumpumzisha, kisha mchezo ambao ulidhaniwa ungekuwa rahisi ya Montenegro,  Rooney angekuwa tayari kuikabili Brom leo kwenye Uwanja wa  Old Trafford.

Lakini, baada ya kurejea Rooney  alionyesha mchezo dhaifu kwenye Uwanja wa Wembley kiasi cha kuzomewa yeye na wenzake.

Kwa sababu hiyo, Ferguson anaweza kumuadhibu kwa kuonyesha utovu wa nidhamu na ukaidi.

Kimsingi, anaweza kumwacha kwa madai kwamba hana kiwango kizuri cha kucheza leo.

Rooney,   25, hajafunga bao lolote kwa Man United tangu  Machi, ingawa msimu huu amefunga moja kwa penalti.

Man United imekuwa na mpango wa kumpa mkataba mpya wa miaka mitano.

Lakini, kuna shaka kwamba huenda asisaini huku Real Madrid ikisubiri kwa hamu kumnyakua.

KUWEPO KWA NYARAKA BANDIA ZA KUPIGIA KURA

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Advocate Nyombi

 

Jeshi la
Polisi mkoani Mbeya, limemkamata na kumfikisha Mahakamani mfanya biashara mmoja ayelitoa taarifa za uongo kuwa katika eneo la Tunduma mpakani mwa Tanzania na Zambia kulikua na gari lililobeba nyaraka bandia na masanduku ya kupigia kura wakati huu wa kampeni na uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika(31 october) mwisho wa Mwezi huu nchini kote.

Kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Advocate Nyombi,  kweli baada ya magari yaliyotajwa kufanyiwa upekuzi wa kina na kutopatikana kwa nyaraka na amemtaja mtuhumiwa huyo kuwa ni Victor Mateni(32), mkazi wa Sikanyihu Tunduma wilayani Mbozi.
Kamanda Nyombi amesema kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo, kumetokana na taarifa zake alizozitoa kwa Mkuu wa Idara ya Forodha mpakani hapo za kuwepo kwa nyalaka hizo kutokua zamasanduku hayo kama ilivyodaiwa na mtuhumiwa huyo.
Amesema “ Jumamanne Oktoba 19, mwaka huu mfanyabiashara huyo alimwendea Bw. Jovitas Kanisha Charles ambaye ni Mkuu wa Idara ya Forodha mpakani hapo na kumwambia kuwa gari lenye namba za usajili T.288 BHR aina ya Iveco likiwa na tela lenye namba T. 966 BKS mali ya Kampuni ya usafirishaji mizigo hapa nchini ya AZANIA lilikuwa limebeba shahasa na mabokisi hayo bandia na vilikuwa vikiingizwa nchini kwa siri”alisema kamanda nyombi.
Amesema Mkuu huyo wa Idara ya Forodha mpakani Tunduma, aliwasilisha taarifa hizo kwa Mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na usalama hapo mpakanai na kuitisha kikao cha dharura kuitathimini taarifa hiyo.
Kamanda Nyombi amesema wakati wa kikao hicho cha dharura kamati hiyo iliamua kufanya upekuzi wa kina katika gari hilo pamoja na tela lake ili kubaini ukweli wa taarifa hizo na kuchukua hatu za kiusalama.
Amesema wakati wa upekuzi huo, kamati hiyo pia ilimshirikisha mtoa taarifa ili naye ashuhudia kitakachopatikana lakini hadi mwisho wa upekuzi kulikuwa hakuna nyaraka ama masanduku ya kupigia kra yaliyobainika.
Amesema gari hilo lilikuwa na bidhaa mbalimbali za madukani ambazo ni za halali kwa kusafirishwa na kwa matumizi. Bidhaa hizo zilikuwa zikisafirishwa kutoka Afrika ya Kusini kwenda kwa wafanyabiashara wawili wa Jijini Dar es Salaam.
Kamanda huyo amesema baada ya upekuzi huo kutobaini kosa walimkamata mfanyabiashara huyo na kumfikisha makahakamani kwa kutoa taarifa za uongo na kesi yake imeahiirishwa hadi itakapotajwa tena Novemba 4, mwaka huu na mtuhumiwa amepelekwa rumande.
Huyo ni mtu wa pili kufikishwa mahakamani katika kipindi kisichozidi wiki moja kwa kutoa taarifa za uongo na kusababidha athari kwa watu wengine na taifa kwa ujumla.
Hata hivyo Kamanda Nyombi amesema makachero wa Polisi mkoani humo wanamsaka mtu mwingine ambaye pia alisaiidia kueneza taarifa za uvumi huo.
Jumanne wiki hii, Mwenyekiti wa Wazee wastaafu wa iliyokuwa Afrika ya Mashariki Nathanael Mlaki, alijisalimisha Polisi Jijini Dar es Salaam na kufikisha Mahakamani kwa madai ya kutoa taarifa za uongo kuwa mmoja ya wazee wastaafu wa iliyokuwa Jumuia hiyo amefariki dunia baada ya kumwagiwa maji ya kuwasha na Polisi wakati walipofunga barabara.

HIGH EDUCATION STUDENTS LOAN BOARD (HESLB) TANZANIA

Bodi inayoshughulikia mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu imetoa majina ya wanafunzi walioomba mkopo kwa vyuo vyote hapa nchini http://www.heslb.go.tz/

MELI YA KICHINA YATUA DAR ES SALAAM NA KUTOA MATIBABU BUREE



MKUU wa Hospitali Kuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Lugalo, Meja Jenerali Salim Salim, akipewa zawadi maalum na Kamanda wa Meli ya China, yenye vifaa na madaktari wa kutoa huduma za matibabu,Bao Yuping, alipotembelea meli hiyo leo katika Bandari ya Dar es Salaam

DCMA receives Roskilde World Music Award 2010!


We are very happy to share the news with you that the Dhow Countries Music Academy has just been announced as the 2010 recipient for the Roskilde Festival World Music Award.

The award is a form of international recognition given to societies or organizations that are creating musical development by emphasizing locally-based music genres - to ensure a cultural stepping stone for children and the youth in the developing world. The award is presented by the Roskilde Festival Charity Society on the background of recommendations from the Roskilde Festival, WOMEX and EFWMF (European Forum of World Music Festivals).

DCMA receives the 30,000 Euro Award for its work on maintaining and developing the musical traditions in an area where cultural development is often relegated to the background because of more basic challenges.

"It is often with good intentions that cultural projects are launched in third world countries. But it’s harder running the projects over a longer period so that they can make a difference that was the aim to begin with. The Dhow Countries Music Academy draws attention not only because of its purpose and level of ambition. It is also a professionally working organization that has proven its worth and managed to make a difference in its area," says Peter Hvalkof, booker of world music at Roskilde Festival, about the background for the choice of the award winner.

The DCMA is the second recipient of this new award which was given out in 2009 to Malian musician Rokia Traore for founding of La Fondation Passarelle - an organization for professionalizing Malian music culture.

"The award is a great honor and encouragement for all of DCMA staff, students and the board. It recognizes many years of hard work in building a new and meaningful institution in the cultural sector and it also pays tribute to the unique beauty of Swahili music and culture and the work of teaching musicians. We hope to put the prize money to the best possible use by enabling and encouraging young students to take advantage of all that DCMA has to offer and discover the beauty and potential of making a career as a musician." (Hilda Kiel, CEO)

The funds received as part of the award will be used exclusively for educational activities by offering study scholarships, purchasing of instruments and study materials and the development of special music programs for children and the youth in schools and in villages.

Until now the school has received both local and international honors for its achievements so far that included the US Ambassador's Fund for Cultural Preservation (2003), The BBC World Music Award for World 'Movers and Shakers' awarded to its current CEO (2007) and The Zanzibar Music Award for special category for the most active arts and culture organization (2007).

Further information of the Roskilde Festival World Music Award 2010:

http://www.womex.com/realwomex/rfwma.html

More information on the WOMEX Awards:

http://www.womex.com/lnk/awards

DCMA CEO and Board Vice-Chairman Adel Dabo will travel to Copenhagen for the award ceremony that will conclude the annual World Music Expo (Womex). The Dhow Countries Music Academy will receive their Award on Sunday, 31 October 2010, 12:00 - 14:00, at the WOMEX Award Ceremony accompanied by a WOMEX Networking Breakfast, both open to WOMEX delegates only.

WOMEX is the world's largest annual exposition for World Music that integrates a trade fair, showcases, conferences, film market, networking sessions and awards taking place from 27-31 October 2010.

DCMA can be contacted at Stand No. 130, ACP Festivals Network.

We hope to see many of you at WOMEX!

With sincere thanks and greetings from the DCMA TEAM.

Thanks to our sponsors and supporters:

Andrew Scrivener Fund

And special thanks to all our local supporters!

Dhow Countries Music Academy
Old Customs House, Mizingani Rd.
Stonetown, Zanzibar
United Republic of Tanzania
Email: admin@zanzibarmusic.org
Tel: +255.24.223 4050 / 77.7416 529
P.O. Box 4055
www.zanzibarmusic.org

 

October 21, 2010

GOD LOVES US


                      GOD            doesn't    love us because we are good;
                   we are good because God loves us and all
                               that we love deeply becomes a part of us.
                           Keep on loving cause we are shaped and fashioned
                                               by what we love.
 

SPEED COOKING

wachina nao!

ELIMU BORA KWA KILA MTANZANIA NA UJENZI WA TAIFA LILILO BORA LA BAADAE

nchi zinazoendelea zinaipa secta ya elimu kipaumbele lakini, tujiulize je hii elimu inayotolewa majengo yanaridhisha?. jionee moja ya jengo, ujiulize kwa staili hii kiwango cha elimu kinaridhisha kwa nchi kama Tanzania?

Waalimu nao hawasiti kuwaambia wanafunzi watafute sehemu yoyote watakayoweza kukaa ili wapate kufundishwa. tujiulize kwa namna hii wanafunzi wataweza kuyamudu masomo yao vyema?

Bila kuwasahau Waalimu, wote tunafahamu watu wa kuheshimiwa sana ni walimu kwani kupitia hawa walimu tunawapata Marahisi, Mawaziri,Wabunge, Maprofesa,Madokta na watu wengi sana walioelimika,  tujiulize maswali machache  hawa walimu wanathaminiwa? wanaishi katika mazingira yanayostahili? Wanapewa posho zao kwa wakati? wanaweza kujiajiri leo au kesho ambayo hawatakuwa katika kazi zao za kutegemea mwisho wa mwezi? Wanaweza kujenga nyumba zao wenyewe? ni hayo tu kuhusu walimu tena hawa ndio wanaostaili kuitwa WAHESHIMIWA!




Tunashangaa kuona hawa wanaojiita waheshimiwa wakiishi katika nyumba nzuri zenye thamani ya mabilioni bila hata kuwakumbuka hawa wenzetu waliosahaulika (walimu) waliowapa elimu, na hiyo elimu wakaitumia kwa manufaa yao wenyewe hii ni aibu na hata kujilimbikizia mali nyingi kama inavyo onyesha ktk picha hapo juu.

Kama sekta ya Elimu ingethaminiwa kama ilivyo sekta nyingine Serikali yetu ingekuwa wapi leo karne ya ishirini na moja? 

Watunga sheria wako wapi? Sheria zilizotungwa nazo zinafuatwa? sheria mnazotunga ni kwaajili ya akina nani?

October 20, 2010

KARIBUNI


NDUGU ZANGU WATANZANIA NA HATA WALE WA NCHI ZA MBALI NAPENDA KUWATAARIFU KUWA NIMEANZISHA BLOG HII IITWAYO {MTAZAMO} KWA NIA NZURI YA KUUHABARISHA UMMA KATIKA NYANJA TOFAUTI KATIKA MAISHA YETU YA KILA SIKU HUSUSANI MAMBO YOTE YA KIUCHUMI, KISIASA NA HATA KIJAMII. KWA HIYO NDUGU ZANGU NAOMBENI USHIRIKIANO WENU KIMAWAZO HATA KIMTAZAMO  KATIKA KUBORESHA BLOG HII ahsanteni!